Monday, October 5, 2009

PESA SIO USHINDI TUNAZAMA UWEZO



Magwiji wa jiji la Madrid, Real Madrid wameonja chungu ya kufungwa kwa mara ya kwanza katika ligi kuu ya soka huko nchini Hispania msimu huu baada ya kukubalia kisago kama si kichapo cha mabao mawili kwa moja toka kwa Sevilla Fc.



Wakicheza nyumbani tena kwa kujiamini kupita kiasi Sevilla FC walipata mabao yao ya ushindi katika dakika ya 33 na 67 kupitia kwa Jesus Neves pamoja na Renato huku bao la kufutia machozi ya Real Madrid likifungwa na Pepe katika dakika ya 49.



No comments:

Post a Comment