Friday, January 22, 2010

msaada jamani



400,000 kuhamishwa nchini Haiti

Serikali ya Haiti imesema kuwa itawahamisha zaidi ya waathiriwa laki nne kutoka mji mkuu wa Port Au Prince kufuatia tetemeko la ardhi la wiki iliyopita.
Waziri wa masuala ya ndani Paul Antoine Bien-Aimé amesema kuwa tayari mabasi yameandaliwa kuwasafirisha waathiriwa hao kutoka mji mkuu hadi vijijini kusini na kaskazini mwa nchi hiyo.
Serikali hiyo imesema kuwa takriban miili 75,000 imezikwa katika makaburi ya pamoja japo inaamini kuwa idadi ya waliofariki ni kubwa zaidi.

No comments:

Post a Comment