Friday, April 30, 2010

Kuzuia ndoa ya wake wengi yazua tafrani

Mswada unaokusudia kupiga marufuku ndoa za wake wengi Malawi umeamsha hasira kali kutoka kwa jamii ya kiislamu nchini humo.
Msemaji wa jumuiya ya kiislamu ya Malawi, Imran Shareef Muhammed, ameiambia BBC mswada huo ukipitishwa utawabagua waislamu wachache waliopo nchini humo.


COMREDY ZUMA ANANDOA YA WAKE WENGI

Bw Muhammed amesema kuna takriban asilimia sita zaidi ya wanawake kuliko wanaume Malawi.

Na iwapo ndoa za wake wengi zikipigwa marufuku, wanawake wengi watabaki bila kuolewa na hivyo kujiingiza katika ukahaba.

Siku ya Alhamisi, waziri wa jinsia wa Malawi alisema hatua ya kupiga marufuku ndoa hizo ni muhimu ili kuzuia wanawake kunyanyaswa katika ndoa za wake wengi.

BBCswahili.com, understand

No comments:

Post a Comment