Sunday, April 25, 2010

THE MANARA CAREER




kassim manara akichachafya enzi hizo. yeye ndiye mdogo katika familia ya soka ya manara, ambapo wote walijaaliwa vipaji vya hali ya juu katika uchezaji na hadi sasa hakuna ukoo uliotoa nyota wengi kwa mpigo kama kina manara. Kassim alichezea Yanga kabla ya kuhamia Pan African na baadaye kwenda ughaibuni ambako yuko hii leo ila kwa sasa kastaafu









Sunday Manara akikata mbuga. Huyu alipewa jina la Kompyuta kwa uwezo wake. Kumbukumbu zinaonesha yeye ndiye mwanasoka wa kwanza kwenda kucheza soka la kulipwa ughaibuni kwa mafanikio makubwa. Hivi sasa amestaafu na yupo nyumbani





Kitwana Manara 'Popat' alianza kama golikipia kabla ya kuamua kuwa mshambuliaji ambapo alitisha sana katika umaliziaji hasa kwa vichwa. Yeye pia amestaafu na anajishughulisha na siasa akiwa diwani na pia mmoja wa washauri kwa shirikisho la soka TFF



Kwa hisani ya issamichuzi.blogspot.com/



No comments:

Post a Comment