Monday, August 31, 2009

UKIWA MZIMA MWAMBIE MUNGU AHSANTE !!!

AHMED KANDORO mtangazaji wa chanel ten na magic fm pia ni mkurugenzi wa shirika la tuwasaidie akizungumza na waandishi wa habari kuomba msaada wa wadau mbalimbali kuhusu watoto wawilia ambao ni walemavu na wanahitaji msaada wa hali na mali watoto hao ni steven peter Luanda mkazi wa kijiji cha Bunduki mkoani morogoro na salma omary mkazi wa kichangani pia wa mkoani morogoro

Huyu ni steven peter Luanda ambaye kwakweli hana miguu hapa kabebwa na bibi yake huyu anaomba msaada wa kusoma tuu kwakweli wapo watu kama mimi ambao wana miguu lakini hawajui kusema shukrani lakini bwana mdogo huyu akasema ahsante.


Huyu ni salama omary amabaye ana miaka ishirini na sita wanasema hajawahi kutoka nje tangu azaliwe ampaka alipofika miaka 24 kwakeli anakipaji cha kushona kama unavyoweza kuona pichani alianza kushona vitambaa kwa kutumia chelewa lakini sasa anashona kwa kutumia sindano digital .
Ukitaka kutoa msaada piga na namba hiii 0713884108




No comments:

Post a Comment